Saturday, May 8, 2021

JIFUNZE HAPA : JINSI YA KUVIVUTA FURSA NA KUZITUMIA NDANI YA MUDA MFUPI.

Unakwama Wapi Mpaka Sasa Hujui Jinsi Ya Kuzivuta Fursa?

Huzioni fursa lakini wenzako wanaziona na kuzitumia je, unajua tatizo ni nini?

Ulichofichwa kwa muda mrefu leo unakwenda kukifahamu na kukitumia ipasavyo.

Angalia huu mfano hapa chini;

MARAFIKI  WAWILI  WAKIVUA.

Kulikuwa kuna wavuvi wawili ambao ni marafiki wa karibu.

Walitumia wikiendi kuvua samaki pamoja.

Pale wanapokuwa wametingwa na shughuli zao na familia zao ilikuwa ngumu kuonana.

Ilikuwa ni siku ya juma mosi waliamua kuongozana  pamoja karibu na ziwa kufurahia shughuli za uvuvi kwenye siku yao.

Wote walibeba nyenzo muhimu za uvuvi pamoja na vikorombezo vingine kwa ajili ya kupikia samaki.

Walifika kwenye bwawa.

Walikaa kwa mbali na kuanza kuwinda samaki.

Mvuvi wa kwanza alipata samaki mkubwa na mzuri ndani ya dakika chache.

Alifurahi akamuweka samaki ndani ya jokofu la plastiki lenye mabonge ya barafu na kumuhifadhi.

Alitumia muda kidogo kuwanasa samaki wengine wachache.

Aliamua kuwapika wachache,

Pia aligandisha samaki wachache na wengine aliwaacha kwa ajili ya kuwapeleka nyumbani.

Ilichukua zaidi ya li saa wakiwa wanavua.

Mvuvi wa kwanza  akamfuata mvuvi wa pili na kumuuliza kama anahitaji msaada.

Mvuvi wa pili akamjibu hapana.

Dakika chache , mvuvi wa pili anakamata samaki mkubwa.

Ata hivyo, alimrudisha tena ndani ya ziwa.

Mvuvi wa kwanza alishangazwa na iko kitendo.  

Mvuvi wa pili akawa ana kamata samaki wakubwa , lakini anawarudisha wote ndani ya maji.

Mvuvi wa kwanza anachukizwa sana na iko kitendo cha mwenzake, anamuuliza kwa hasira “ Una wazimu?

Kwanini unawarudisha samaki wote ndani ya maji?

Walikuwa wazuri na wakubwa.

Mvuvi wa pili anajibu, “ Najua walikuwa wakubwa, bali sina kikaango kikubwa cha kupikia hao samaki wakubwa.

Kwa hiyo natafuta samaki wadogo ambao wataenea kwenye kikaango changu kidogo.

Akasema mungu ananisumbua sana leo.

Baada ya kusikia hilo, mvuvi wa kwanza anashangazwa na hilo jibu.

Anamshauri mvuvi wa pili kumkata samaki mkubwa vipande vipande ili aweze kuenea kwenye kikaango na wapike bila shida.

Somo;

Watu wengi wapo kama mvuvi wa pili.

Wanazungukwa na fursa nyingi lakini wanashindwa kuzitumia , na hii ni kwa sababu hawazioni  na hawajui jinsi ya kuzivuta.

Wanachokiona ni vikwazo, uchache, matatizo na hatari ya kupoteza.

Ata wewe mwenyewe unajishangaa unazungukwa na fursa nyingi lakini unashindwa kuziona na kuzitumia, lakini wenzako wanaziona na kuzitumia.

Na hiki ndicho kinachowatofautisha matajiri na maskini.

Matajiri wanajua jinsi ya kuzivuta fursa na kuzitumia ipasavyo lakini masikini wanafanya kinyume chake.

Ata wewe leo hii unaweza kujifunza jinsi ya kuzivuta fursa na kuzitumia ndani ya muda mfupi.

Kwa kusoma na  kujifunza , unakwenda kujifunza jinsi ya kuzivuta fursa na kuzitumia ndani ya muda mfupi.

Unakwenda kufahamu vizuizi vinavyokuzuia usizione  fursa.

Karibu sana UJIUNGE  NA    " DARASA  ONLINE "--ujifunze  TABIA ZA KITAJIRI na FURSA  MBALIMBALI   ZINAZOKUZUNGUKA  na Mengine  mengi  YANAYOHUSU FALSAFA , SAIKOLOJIA, MAHUSIANO ,

Ujifunze kwa kina na kuyaelewa maarifa haya muhimu sana kwako,

 Kisha uchukue hatua ili maisha yako yaweze kubadilika, ufike kwenye utajiri, mafanikio na furaha.

 

Kwa  Maelekezo  Tuwasiliane 

NA  KOCHA   MWL.  JAPHET  MASATU

WhatsApp + 255 716 924 136 ,  + 255 755 400 128 

EMAIL : japhetmasatu@gmail.com

 

JINSI YA KUPATA WAZO LA BIASHARA ILI LIWEZE KUKULETEA MAFANIKIO MAKUBWA SANA--NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU----( PDF )

JINSI YA KUPATA MTAJI WA BIASHARA NA VYANZO VYAKE------NA KOCHA MWL. JAPHET MASATU----( PDF )

Saturday, March 6, 2021

JINSI YA KUJIJENGEA BAHATI YA MAFANIKIO KWENYE MAISHA YAKO.

Watu wote ambao wanafikia mafanikio makubwa, huwa kuna bahati wanazokutana nazo kwenye safari yao ya mafanikio, japo siyo wote wanaoziona. Na pia bahati hizo haziwafuati kitandani wakiwa wamelala, badala yake wanakutana nazo wakati wanapambana.




Naval Ravikant anasema kuna aina kuu nne za bahati;

Aina ya kwanza ni bahati kipofu, hii ni pale mtu anapokutana na bahati ambayo hakuitegemea kabisa kwenye maisha yake. Mfano unatembea barabarani na kukutana na jiwe la dhahabu, hiyo ni bahati ambayo imekutokea tu, hakuna namna unaweza kujisifu umechangia kuipata.

Aina ya pili ya bahati ni ile inayotokana na mtu kuweka juhudi na ung’ang’anizi kwenye kile anachofanya. Hapa mtu anakuwa amechagua kufanya kitu, lakini anakutana na changamoto na vikwazo ambavyo hajui hata atavivukaje, lakini hakati tamaa, anaendelea kuweka juhudi na baadaye anakutana na fursa nzuri inayomwezesha kufanikiwa. Bahati hii inatengenezwa kwa sababu kama mtu angekata tamaa mapema, asingekutana nayo.

Aina ya tatu ni ile inayotokana na ujuzi maalumu, ambapo mtu unakuwa na uwezo wa kuona kitu ambacho wengine hawakioni. Kuna watu wanaona vitu ambavyo wakivifanyia kazi, vinawapa matokeo makubwa na kwa wengine inaonekana ni bahati. Bahati ya aina hii inaweza kutengenezwa, hasa kwa mtu kujipatia ujuzi ambao wengine hawana.

Aina ya nne ni pale unapojijenga sifa ya kipekee ambapo bahati inakufuata mwenyewe. Aina hii ya bahati ni ngumu kwa sababu mtu unakuwa umejijengea sifa fulani ambayo kwa sasa unaweza usione matumizi yake, lakini siku moja kikatokea kitu ambacho hakuna anayeweza kukifanya, ila wewe kwa sifa uliyonayo, ndiye pekee unayeweza kufanya na hapo ukapata fursa kubwa. Kujenga aina hii ya nne ya bahati, jua ni kitu gani unacho ambacho wengine hawana, kisha kiendeleze na jijengee sifa kwenye kitu hicho. Na ipo siku usiyoijua, watu watakutafuta uwasaidie kwenye kitu hicho na watakuwa tayari kukupa chochote unachotaka.

Jinsi ya kujijengea bahati.

Ukiachana na aina ya kwanza ya bahati ambayo inatokea bila wewe kujua, aina tatu za bahati unaweza kujijengea kwenye maisha yako.

Na unaweza kufanya hivyo kupitia kujijengea sifa ya kipekee kupitia kile unachotaka kufanikiwa.

Na sifa ya kwanza muhimu kabisa unayopaswa kujijengea ni kuwa mtu wa kufanya na siyo tu kupanga na kuahidi.

Wengi kwenye maisha huwa wanaweka malengo makubwa, wanakuwa kabia na mipango ya kufikia malengo hayo, lakini inapokuja kwenye kuchukua hatua, ndipo wanaofanikiwa na wanaishindwa wanapotofautiana.

Wanaoshindwa huwa ni watu wa kutafuta sababu kwa nini hawawezi kufanya na hata wanapoanza ni rahisi kuahirisha.

Lakini wale wanaofanikiwa, wanaposema wanafanya, wanafanya kweli, ni watu wa matendo na siyo maneno pekee, siyo watu wa kutoa sababu, bali ni watu wa kutoa matokeo.

Hivyo kama unataka kujijengea bahati itakayokufikisha kwenye mafanikio, chagua eneo unalotaka kufanikiwa na chukua hatua kila siku. Siyo kupanga pekee, bali kuchukua hatua kila siku.

Kwa kuchukua hatua kila siku, unajiweka kwenye nafasi kubwa ya kukutana na bahati kuliko yule asiyechukua hatua kabisa au anayechukua hatua pale anapojisikia pekee.

Kufanya siyo rahisi, hasa kwa namna ambavyo wengi wamejijengea tabia kwenye maisha yao. Hivyo hii ni tabia unayopaswa kuweka juhudi kubwa kwenye kuijenga.

Kwa wengi, kufanya kila siku siyo kitu wanachoweza kujisimamia na wakakikamilisha.